VITU NILIVYOJIONEA NIKIWA NDANI YA NCHI YA CONGO

Tangu nisafiri kuja Congo kuna mambo fulani ambayo nimejaribu kuona kwa macho yangu mengine kwa hisia tu. Pia kuna baadhi ya mambo ambayo nimeyafanyia utafiti mdogo na baada ya hapo nikajiridhisha kwa vitendo. Ngoja niweke ambayo nilijionea mwenyewe:-

1. Ukiwa Mtanzania utalala na wengi:
Hapa nazungumzia kwa wale wenzangu nami wanaependa kuserereka na totoz, yaani ni kwamba wanapoona unazungumza kiswahili fasaha hujipendekeza na kuwa na wewe karibu. Hauna haja ya kuanza kutingoza mda mrefu ni kuomba namba ya sim na mengine yatajileta yenyewe.

2. Kuna wadada wazuri mno ila wengi ni makahaba:
Hapa sijajua sababu kuu ni ipi ambayo inapelekea wadada wazuri wanapenda kazi hiyo.
Unapishana na wadada kama watatu wanne utakaemkuta usiumize kichwa chukua twende.

3. Boda boda nyingi:
Yaani kuna boda boda nyingi kuliko nchi zingine zote za afrika. Hapa naweza kusema kumechangiwa na wingi wa watu wenyewe na nchi yenyewe ilivyo kubwa.

4. Chakula safi ni shida:
Kwa Mtanzania ambae umezoea vitu vizuri vizuri kwe 'restaurants' za Tz basi kwa huko utazunguka sana mwisho was siku utaambulia ugali (bada). Chapati zao sio nzuri hawajui kupika supu hata samaki was kwao.  Siku Mtz akijitokeza kupika pilau au biriani basi ataondoka na utajiri usio na kifani.

5. Wanapenda kujichubua sana:
Kwao ni vitu vya kawaida na imeonekana 'fashion' kufanya hivyo mafuta yanayokatazwa Tz, Congo yapo sokoni.

6. Wanathamini dola kuliko hela ya kwao:
Yaani kila duka utakalotembelea ni dola dola hadi unachoka mwenyewe. Sio kwamba hela ya kwao hawatumii, la hasha! Wanatumia sana ila dola ndo kila kitu mijini na vijijini.

7. Kiswahili wanakipenda sana:
Mara nyingi wanapenda kuongea kiswahili kuliko kilingala na kizulu. Hata kama utawakuta wapo wenyewe wanaongea lakini lazima waingize kiswahili. Kiswahili walikipenda sana ila kifaransa kiliwapenda zaidi.

8. Pombe ni nyingi sana kuliko maji safi ya kunywa.
Hapa kila kona utakayozunguka utakuna na pombe aina ya bia zimesheheni, lakini ukija kwa upande wa maji ya kunywa sio mengi. Kwa leo niishie hapo maana kuna mengine nimeyasahau ila kama kuna mtu ambae anafaham zaidi anaweza kujazia nyama.

Image result for animated download now gif

No comments

Powered by Blogger.