NJIA SAHIHI ZA KUACHANA NA MPENZI WAKO KWA AMANI

Mdau wetu ameainisha njia zifuatazo kuwasaidia wadau kumaliza mahusiano na wenzi wao kwa amani.

1. Kuwa na Uhakika na unachotaka kufanya: Kama huna uhakika juu ya hisia zako kwa mwenzi wako unapotaka kuvunja uhusiano bora usifanye hivyo maana utafanya moyo wako usiwe na maamuzi dhabiti.

2. Fikiria Sababu za Kuvunja Uhusiano: Unapojua sababu zinazopelekea wewe kuvunja mahusiano itakusaidia kutoa majibu ya uaminifu pale unapoulizwa.
3. Maliza Mahusiano wewe Binafsi: Kama umekuwa na mpenzi wako kwa muda mrefu au kipindi chochote uliwekeza muda na nguvu zako za kujenga mapenzi, basi ni busara mahusiano hayo ukayamaliza mwenyewe.

4. Msikilize mwenzi wako: Hata kama umeshaamua huwezi kubadili mawazo juu ya kuvunja mahusiano yenu haina maana kuwa usimsikilize mwenzi wako.

5. Kuwa Mtulivu na Makini: Unahitaji kuumaliza uhusiano na kuondoka mahali mlipo. Hata hivyo ni busara kuwa mtaratibu na mpole.

Je, nini uzoefu wako kuhusu kuacha au kuachwa katika mahusiano?

Image result for animated download now gif

No comments

Powered by Blogger.