MFAHAMU BOBRISKY. SHOGA TAJIRI NA MAARUFU ZAIDI NCHINI NIGERIA

Shoga maarufu kutoka pande za +234 nchini Nigeria, Idris Okuneye (28), maarufu kama BOBRISKY, ndiye staa shoga aliyeamua kujiweka wazi nchini Kwao kwa kuvaa na kuishi kama mwanamke, unaambiwa hutumia mamillion ya pesa kujiremba na ku maintain muonekano wa kike. 

Shoga huyo ambaye pia ni rafiki wa muigizaji mkongwe, Tontoh Dikeh, amekua akivutia watu mbali mbali kwa umahiri wake wa kujiremba na kuishi maisha expensive pengine kuliko mastaa wengine nchini humo.
Bobrisky anajihusisha na biashara ya vipodozi ambayo anadai ndo iliyompa utajiri wa kutisha mpaka sasa, ingawa hata yeye mwenyewe pia amewahi kusema mara kwa mara kuwa anatoka na ma politician na watu wazito wenye pesa zao nchini humo ambao pia wanampa jeuri ya kuishi maisha ya kifahari huko Lagos state.

No comments

Powered by Blogger.