KILA MTU HUFANYA HIVI HASA AKIWA AMECHOKA


1.Kuingia kwenye chumba halafu ghafla unasahau uliingia kufanya nini, ukiamua kutoka tu, unakumbuka!

2.Kuangalia saa na baada ya kuondoa macho tu kwenye saa, unasahau ilikuwa saa ngapi! Na inakubidi uangalie tena!

3.Kukubaliana na mtu kwa kutikisa kichwa kumbe hata hujasikia kakuambia nini. Unaombea tu asije akawa amekuuliza swali.

4.Unatembea katikati ya watu mara ghafla unagundua umekosea njia, Unajidai umesahau kitu au kuangalia simu yako na kuanza kurudi kwa kasi!

5.Unabishana kichwani kwako mwenyewe mpaka unapata hasira, baadae unagundua ni mawazo tu na kujiona mjinga!

6. Betri za rimoti yako zimekwisha unaamua kuminya batani za rimoti kwa nguvu zaidi ukihisi itasaidia!

7.Unaambiwa kitu Fulani ni cha moto, unaamua kugusa na unaungua kweli!

8. Unajikwaa au kujigonga sehemu na unaanza kutukana ukihisi sehemu hiyo inakusikia.

9 Kujiangalia kwenye kioo cha jengo na kusahau kuwa kuna watu ndani ya jengo na wanakuagalia.

10. Unabisha kwamba hujalala (huko usingizini) na unasikia kila kinachoongelewa, kumbe kila mtu ameshakushtukia!

No comments

Powered by Blogger.